Search
Free School Management System
Free School Management System for Kenya

Free School Management System

Learn More

KCSE CLUSTER TESTS 26

Kiswahili Paper 3

SEHEMU YA A (Alama 20)

Riwaya-S. A. Mohamed: Utengano
1.


LAZIMA
“Kumbe bwana wewe mjinga eeh. Yupo mtu asiyejua siasa dunia hii? Wandanganye hao wasiokujua, mimi nakujua vilivyo.”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)

b) Onyesha inavyodhihirika kuwa hapana asiyejua siasa dunia hii (alama 8)

c) Thibitisha kuwa mnenaji anamjua mnenewa vilivyo (alama 8)

20 marks

SEHEMU YA B (Alama 20)

Tamthilia-Kithaka wa Mberia: Kifo kisimani
2.

“Bahati nasibu inapomteremkia mtu, mara nyingine uhalisia huonekana kama ndoto,
mambo huwa hayaeleweki kwa urahisi’’
i) Fafanua muktadha wa dondoo hii. (alama 4)

ii) Onyesha bahati inayorejelewa katika dondoo hii. (alama 4)

iii) Eleza jinsi ambavyo watu wengine katika tamthlia walikosa kuteremkiwa na bahati nasibu (alama 12)

20 marks

SEHEMU YA C (Alama 20)

Hadithi fupi-K. W: Wamitila: Mayai waziri wa maradhi na hadilti nyingine
3.

Jibu swali la 3 au la 4
3. ‘Kweli ibilisi wa mtu ni mtu! Thibitisha kauli hii kwa kurejelea hadithi zifuatazo (alama 20)
i) Tuzo
ii) Pwaguzi
iii) Msamaria
iv) Kachukua hatua nyingine
4 “……………Katika ukurasa huu aliona picha ya mamake……………………..’’
i) Mbali na picha hii, eleza picha nyingine tano alizoziona. (alama10)

ii) Hadithi ‘Mayai waziri wa maradhi’ inamulika matatizo mbalimbali yanayozikabili nchi nyingi za kiafrika. Thibitisha kauli hii kwa kufafanua matatizo yoyote matano. (alama 10)

20 marks

SEHEMU YA D (Alama 20)

Ushairi
4.


5. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali

Wangu niliyekupenda, leo nitakufukuza

Kuishi umenishinda, waniletea mayaza

Ola vile nimekonda, jasadi nimepooza

Uwache kuniumiza,ni heri mwana kunenda


Ulikuwa wangu nyonda, huba nikaikoleza

Kukupenda kama tunda, embe lenye uliwaza

Ukajigeuza punda, teke umenicharaza
Uwache kuniumiza, ni heri mwana kunenda


Nimekonda kama ngonda, mwandani wanilemaza

Sautiyo ya kinanda, sitaki kusikiliza

Sikutaki bora kwenda, muhibu wanishangaza

Uwache kuniumiza, ni heri mwana kunenda


Mengi ulionitenda, si madogo yakupuza

Nalikupa kila gwanda, uvae na kupendeza

Ulikula na kuwanda, kadiri ulivyoweza

Uwache kuniumiza, ni heri mwana kunenda.


Kinyume ulipokwenda, nilidhani kuteleza

Na wewe hukujilinda, nyendo mbaya kupunguza

Cha kuvunda kisha vunda, hata ukikifukiza

Uwache kuniumiza, ni heri mwana kunenda


Mja wewe wanishinda, kwa tama wachukiza

Kila kitu unadanda, kingawa cha kuumiza

Huwi ndani ya kibanda, huishi kujitembeza

Uwache kuniumiza, ni heri mwana kunenda

a) Eleza maana ya mleo wa ubeti wa kwanza (alama 2)

b) Fafanua umuhimu wa kipokeo cha shairi hili (alama 2)

c) Eleza sifa za kiarudhi katika ubeti wa tatu (alama 4)

d) Taja methali inayodokezwa katika ubeti wa tano wa shairi hili (alama 2)

e) Eleza maudhui ya ubeti wa pili wa shairi hili. (alama 2)

f) Ni jambo lipi zuri ambalo mshairi atalikosa? (alama 1)

g) Andika ubeti wa sita wa shairi hili katika lugha nathari (alama 4)

h) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi . (alama 3)

i) Mayaza

ii) gwanda

iii) Kuwanda

20 marks

SEHEMU YA E (Alama 20)

Fasihi simulizi
5.

Jibu swali la 6 au 7

6 a) Ni nini maana ya maigizo katika fasihi simulizi. (alama 2)


b) Fafanua aina mbili kuu za maigizo (alama 4)


c) Taja sifa zozote tano za maigizo. (alama 10)


d) Eleza dhima zozote nne za maigizo (alama 4)


7 a) i) Taja njia zozote tatu za ukusanyaji wa data katika fasihi simulizi. (alama 3)


ii) Taja mbinu zozote tatu zinazotumiwa kuhifadhi fasihi simulizi huku ukionyesha umuhimu wa kuhifadhi fasihi hii. (alama 7)


b) Eleza maana ya ushairi kwa mujibu wa fasihi simulizi. (alama 1)


ii) Ni nini maana ya mashairi yafuatayo. (alama 4)


i) Mashairi ya kifunga nyama


ii) Waadhi


iii) Eleza sifa za ushairi simulizi (alama 8)

20 marks

Back Top