Search
Free School Management System
Free School Management System for Kenya

Free School Management System

Learn More

KCSE CLUSTER TESTS 25

Kiswahili Paper 3

1. SEHEMU YA A (Alama 20)

FASIHI SIMULIZI
1.

a) Eleza maana ya miviga kisha uonyeshe inakotumika. (alama 10)

b) Nini umuhimu wa miviga ? (alama 10)

20 marks

SEHEMU YA B (Alama 20)

Tamthilia
2.

Jibu swali la2 au la 3.

2. Eleza jinsi jina mstahiki Meya ni kinyume na matarajio. (alama 20)

3. ‘’Tumechoka kuumbuliwa. Miaka yote tulifanya kazi na hatuoni matunda yake’’.

a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

b) Eleza malalamishi ya mzungumzaji na alioandamana nao. (alama 16)

20 marks

SEHEMU YA C. (Alama 20)

RIWAYA : Utengano
3.

Utengano Jibu swali la 4 au la 5.

4. ‘’Sikutaraji kwamba mambo yatokuwa wao kiasi hiki. Tumefuzu shoga’’……………

a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama

4) b) Eleza yale mzungumzaji na msemewa waliyokuwa wamefuzu kwayo. (alama 16)

5. Huku ukirejelea riwaya ya utengano, taja na ueleze matatizo kumi yanayokumba mataifa yanayoendelea barani Afrika. (alama 20)

20 marks

SEHEMU YA D (Alama 20)

Ushairi
4.

Jibu swali la 6 au la 7.

6. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.

Abdulatif Abdalla: Chema hakidumu


Chema hakidumu, kingapendekeza,

Saa ikitimu, kitakuteleza

Ukawa na hamu, kukingojeleza

Huwa ni vigumu, kamwe hutaweza


Chema sikiimi, kwamba nakitweza,

Japo mara tumbi, kinshaniliza,

Na japo siombi, kipate n’ongeza,

Mtu haniambi, pa kujikimbiza.


Chema mara ngapi, kiniondoka,

Mwanangu yu wapi ?,

Hakukaa mwaka, Kwa muda mfupi, aliwatilika,

Ningefanya lipi, ela, kumzika?

Chema wangu Poni, kipenzi nyanyangu,

Hadi siku hini, yu moyoni mwangu,

Yu moyoni ndani, hadi kufa kwangu,

Ningemtamani,hatarudi kwangu.

a) Eleza bahari za shairi hili. (al.6)

b) Eleza umbo la beti mbili za mwisho. (al.4)

c) Eleza maudhui ya shairi hili. (al.2)

d) Toa mfano wa matumizi ya mbinu ya tabdila katika shairi hili (al.2)

e) Eleza maana ya maneno haya jinsi yalivyotumiwa

i) Ningemtamani

ii) Kitakuteleza

iii) Kinshaniliza

iv) Ela

v) Alojipa tabu

vi) Hini

7. Weusi likosa nini

1) Sie watu weusi, lipataje weusi?

2) Kila kitu kibaya, hupewa sifa mbaya

3) Sifa hii ‘eusi’, yaleta wasiwasi.

4) Rangi hii hakika, ni wapi litoka?

5) Ibada za mweusi, harusi kuzitusi.

6) Kama mtu mweusi, Lusifa ni mweusi.

7) Ibada ya weupe, hupokewa peupe.

8) Adamu naye Hawa, weupe walipewa

9) Yesu mwana wa Mungu, alikuwa Mzungu.

10) Malaika wa Mungu, daima wazungu.

11) Mweusi ti hatendi, silaumiwe pindi.

12) Mweusi duniani, likosa kitu gani?

13) Mweusi jilaumu, measi yako damu.

14) Mweusi umeiga, hata ya kutoiga.

15) Asojali mkuu, atavunjika guu.

16) Baa mejitakia, nani takulilia ?

a) Hili ni shairi la aina gani ? (al.2)

b) Eleza umbo la shairi hili (al.8)

c) Eleza jinsi mtunzi alivyotumia uhuru wa kishairi (al.6)

d) Eleza maudhui ya shairi hili. (al.4)

20 marks

SEHEMU YA E (Alama 20)

Hadithi fupi-Damu Nyeusi : Ken Walibora
5.


8. ‘’Nani ndugu yako’’ ?
a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (al.4)

b) Eleza dhana waliyokuwa nayo watu wa Marekani kuhusu watu Waafrika. (al. 16)

20 marks

Back Top