Search
Free School Management System
Free School Management System for Kenya

Free School Management System

Learn More

KCSE CLUSTER TESTS 19

Kiswahili Paper 3

1.SEHEMU A: (Alama 20)

FASIHI SIMULIZI
1.

a) Eleza isitilahi zifuatazo za fasihi simulizi. (al.4)

i) Ngomezi

ii) Tarihi

iii) Miviga

iv) Mapisi
b)

i) Misimu ni nini? (al.2)
ii) Taja sifa zozote mbili za misimu. (al.2)
iii) Andika mifano miwili ya misimu . (al. 2)
c) Taja matatizo yoyote matano yanayoikabili Fasihi simulizi katika ulimwengu
wa leo. (al.5)
d) Taja sifa zozote tano za jagina. (al.5)

20 marks

2. SEHEMU B: (Alama 20)

RIWAYA S.A MOHAMED
2.

‘’Kumbe bwana wewe mjinga eeh. Yupo mtu asiyejua siasa dunia hii? Wadanganye hao wasiokujua, mimi nakujua vilivyo’’.

a) Eleza muktadha wa maneno haya. (al. 4)

b) Onyesha inavyodhihirika kuwa ‘’hapana asiyejua siasa dunia hii’’. (al.8)

c) Thibitisha kuwa mnenaji anamjua mnenewa vilivyo. (al.8)

20 marks

3.

‘’Msiba wa kujitakia hauna kilio’’.Ukizingatia wahusika wowote watano kutoka riwaya ya ‘’Utengano,’’thibitisha ukweli wa kauli hii. (al.20)

20 marks

3.SEHEMU C: (Alama 20)

TAMTHILIA
4.

Jadili maudhui yafuatayo kutoka tamthilia ya ‘’Mstahiki Meya’’. (al.20)

i) Uongozi mbaya.

ii) Umaskini.

iii) Utabaka

iv) Usaliti.

v) Ukombozi

20 marks

5.

Au
‘’Ndugu wafanya kazi wenzangu tumefika hapa tukiwa kitu kimoja....tumedhalilishwa vya kutosha....................’’

a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (al.4)

b) Fafanua sabau kuu zilizosababisha tukio linalosababisha maneno haya. (al.4)

c) Eleza jinsi tatizo zima linavyoshughulikiwa kufikia mwishoni mwa tamthilia. (al.12)

20 marks

4.SEHEMU D: (Alama 20)

HADITHI FUPI
6.

. Fafanua kikamilifu jinsi maudhui ya ubaguzi wa rangi na ubaguzi kwa ujumla yanavyoendelezwa katika hadithi ya ‘’Damu Nyeusi.’’

Au

20 marks

7.

‘’Utanioa lini?’’.....alimuuliza. ‘’

Utakapojifungua...................alimjibu.

a) Eleza muktadha wa maneno haya. (al.4)

b) Eleza masaibu yaliyompata aliyeuliza swali na hatima yake. (al.10)

c) Taja na ueleze maovu matatu ya kijamii yaliyoibuka katika hadithi hii. (al.6)

20 marks

5. SEHEMU E: (Alama 20)

USHAIRI
8.

a) Linganisha bahari za shairi A na B (al.4)

b) Andika ubeti wa pili wa shairi B kati lugha nathari. (al.4)

c) Taja na utoe mifano miwili ya tamathali za usemi zilizotumika katika mashairi yote mawili. (al.4)

d) Taja na utoe mifano miwili idhini ya mtunzi uliotumika katika mashairi yote mawili. (al.4)

e) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika mashairi. (al.4)

i) Ja

ii) Sharuti

iii) Utukufu

iv) Baidi

20 marks

Back Top