Search
Free School Management System
Free School Management System for Kenya

Free School Management System

Learn More

2015 KCSE Starehe Boys Centre Mock

Kiswahili Paper 3

SEHEMU A: (Alama 20)

FASIHI SIMULIZI
1.

(a) Eleza tofauti kati ya ngoma na ngomezi. {alama 4}

b) Eleza umuhimu wa ukusanyaji wa data za Fasihi Simulizi. {alama 6}

c) Andika fani zilizounda methali zifuatazo:- {alama 3}

i) Chelewa chelewa utapata mwana si wako.

ii) Ujana ni moshi ukienda haurudi.

iii) Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza.

d) Onyesha jinsi methali ni utanzu tegemezi kwa kueleza miktadha ambapo hutumiwa.

{alama 6}

e) Eleza maana ya semi. {alama 1}

f) Eleza maana ya lakabu. {alama 2}

g) Taja sifa 5 za lakabu. {alama 5}

20 marks

SEHEMU B (Alama 20)

RIWAYA: KIDAGAA KIMEMWOZEA Ken Walibora
2.

“Wachache hawa hawaogopi, ashakum si matusi, hata kutema mate au kumwaga

mkojo usoni mwa haki, usawa na uhuru uliopiganiwa na kumwagiwa damu…”

a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

b) Tambua mbinu ya lugha iliyotumika katika dondoo hili. (alama 2)

c) Huku ukitoa mifano fafanua aina 7 za ukiukaji wa haki katika riwaya

ya Kidagaa Kimemwozea.

20 marks

3.

Jadili kauli kwamba Kidagaa Kimemwozea ni riwaya tatizo.

20 marks

SEHEMU C (Alama 20)

TAMTHILIA: MSTAHIKI MEYA Timothy M. Arege
4.

”………Naona unajaribu kutia kidole chako katika mzinga wa nyuki. Ni hatari!”

a) Fafanua muktadha wa dondoo hili. (alama 4)

b) Eleza sifa nne za mnenewa. (alama 4)

c) Bainisha tamathali moja ya usemi inayojitokeza katika dondoo hili. (alama 2)

d) Fafanua mifano mingine mitano ya tamathali hii katika tamthilia. (alama 10)

20 marks

5.

Mwandishi wa tamthilia ya Msitahiki Meya ameshughulikia maudhui ya Usaliti na Ukoloni maomboleo vilivyo. Jadili…

20 marks

6.

MKE WANGU

“Lo! Ati mimi nikachome mihogo niuze! Si nitaonekana nina wazimu mie?”

a) Eleza muktadha wa usemi huu. {alama 4}

b) Jadili sifa za msimulizi kama zinavyojitokeza katika hadithi hii. {alama 16}

20 marks

7.

DAMU NYEUSI

“Nasikia wasichana wenu wote mnawakeketa na kuwashona ili kuzuia ukware?”

a) Eleza muktadha wa usemi huu. {alama 4}

b) Thibitisha jinsi ubaguzi ulivyoendelezwa katika hadithi hii, kwa kurejelea mifano MINANE.

{alama 16}

20 marks

SEHEMU D (Alama 20)

HADITHI FUPI: DAMU NYEUSI NA HADITHI NYINGINE

SEHEMU E (Alama 20)

USHAIRI: Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata.
8.

Kimya changu kimezidi, navunja yangu subira,

Merejeya kwa miradi, kuhitimisha dhamira,

Kukejeli sina budi, niwafunze utu bora,

Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?

Sirikali bila hadi, ndo kiini cha madhara,

Yanopiga kama radi, isokuwa na ishara,

Yamini kuwa gaidi, wakitupora mishahara,

Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?

Wamejifanya hasidi, wasopatana kifikra,

Wana yao maksuudi, kujizombea ujira,

Wakilenga kufaidi, tumbo zao za kichura,

Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?

Nchi yetu kufisidi, ni jambo linonikera,

Tangia siku za jadi, ufukara ndo king’ora,

Kutujazeni ahadi, nyie mkitia fora,

Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?

Maskini watozwa kodi, wapwani na walo bara,

Kwa uvumba na uudi, mwawalipa kwa hasara,

Hamudhamini miradi, mejihisi masogora,

Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?

Mesema kazi ni chudi, basi sirikali gura,

Nafsi zenu mzirudi, mkubali kuchakura,

Makondeni mkirudi, muondoe ufukara,

Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?

Ujanjenu umezidi, demokrasia bakora,

Debeni takaporudi, michirizi kwenye sura,

Kuwachuja a! muradi, kwa za mkizi hasira,

Nani aali zaidi, Wakenya au vinara?

Maswali

(a) Toa anwani mwafaka kwa shairi hili. (alama 1)

(b) Ainisha shairi hili kwa jinsi tatu na kutoa sababu. (alama 3)

(c) Onyesha mbinu za lugha katika shairi hili. (alama 2)

(d) Bainisha matumizi matatu ya uhuru wa mshairi katika shairi hili. (alama 3)

(e) Andika ubeti wa nne katika mtindo tutumbi. (alama 4)

(f) Fafanua maudhui matatu yanayojitokeza katika shairi hili. (alama 3)

(g) Taja mpango mmoja unaotajwa kama njia ya kutatua matatizo ya nchi. (alama 1)

(h) Eleza muundo wa shairi hili. (alama 3)

20 marks

9.

Ajaye kisimani mbele,hunywa maji maenge

Asinywe yalo na vunju

Yakampa kigegezi

Yakamtibua roho akaona na kinyaa

Awali ndio awali awali mbovu hamna

Ikiwa utalimatia,

Utayaramba makombo

Uvidata viyu cheche

Kisoma aali kikupe kisogo

Inajuzu ujihimu

Mwanafuu darasani

Uraukapo bukrata

Katu hutayaramba makombo

Hutokosa kisebeho

Dereva nawe utingo

Natija ni asubuhi

Wateja utawawahi

Wasaa kuzingatia

Uwafikishe kazini

Kwa wasaa ufaao

Wasije wakateteshwa na

Bosi wao nao wakuapize

Nawe mwana zaraa

Mpini uukamate kabla

Jua kutiririsha majasho jasadini

Ushindwe kung’oa magugu

Kutoka kwa lako konde

Mhadimu mwenye zohali

Yajuzu ujihimu

Maziwa anunue majogoo

Usije ukayadata na hivyo

Ukaandaa chai mkandaa

Wateja wakuambae mithili ya ibilisi

MASWALI

a) Lipe shairi hili kichwa mwafaka (alama 1)

b) Shairi hili ni la aina gani (alama 2)

c) Tambua tamathali zozote mbili za usemi zilizotumiwa na mtunzi. (alama 4)

d) Andika ubeti wa kwanza kwa lugha nadhari. (alama 4)

e) Wafanyikazi waliolengwa wataathirika vipi endapo hawatafuata ushauri wanaopewa kwenye shairi? (alama 3)

f) Eleza maana ya maneno yafuatayo. (alama 2)

i) Wakuapize

ii) Jasadini

g) Eleza nasaha yoyote inayotolewa kwa wafanyikazi wowote watatu. (alama 4)

20 marks

Back Top