Kiswahili Paper 1 Marking Scheme
KCSE CLUSTER TESTS 26
Kiswahili Paper 1
i) Hii ni insha ya ripoti
ii) Sura ya ripoti izingatiwe
a) Anwani
b) Utangulizi
c) Mapendekezo
d) Tamati
iii) Mtahiniwa ashughulikie sehemu hizi nne
iv) Maudhui – ni katika sehemu ya mapendekezo
v) Sura ya ripoti lazima ionekane.Mtahiniwa asipotumia sura ya ripoti atakuwa amejitungia swali apate alama ya D- (02)
vi) Akiacha sehemu mbili za sura aondolewe maki 4s
vii) Iwapo mtahiniwa atashughulikia sehemu zingine za ripoti kama vile : yaliyoshugulikiwa na kamati, utaratibu uliotumiwa na matokeo ya uchunguzi hataadhibiwe litakuwa ni swala la mtindo lakini maudhui yawe tu katika sehemu ya mapendekezo
Majibu yanayotarajiwa:
i) Kuwa na michezo ya pamoja
ii) Kuwa na mikutano kati ya viongozi inayoshughulikia kuleta umoja wa makabila
iii) Matatizo yao yashughulikiwe kwa pamoja
iv) Chanzo cha migogoro kichunguzwe
v) Viongozi wawe mstari wa mbele kuondoa ukabila n.k
vi) Watu wa sehemu mbalimbali waimarishe utangamano kupitia ndoa, biashara n.k
vii) Sera ya kusajili wanafunzi katika shule za upili iwaruhusu wanafunzi kutoka sehemu tofauti tofauti kujiunga na shule yoyote nchini
viii) Viongozi wanaochochea ukabila wachukuliwe hatua kali
ix) Lugha za kienyeji zisitumike mahali pa kazi
x) Vituo vya utangazaji vinavyotumia lugha za kienyeji vipigwe marufuku. Tathmini hoja za mtahiniwa
20 marks
2 i) Hii ni methali
ii) Mtahiniwa atoe kisa au visa kuthibitisha
iii) Methali ina pande mbili kwa hivyo mtahiwa ashughulikie pande zote mbili
iv) Akijibu upande mmoja atakuwa amejaribu kujjibu swali kwa hivyo asipite kiwango cha C (08)
v) Maana – Taa ni samaki ambaye ana kinywa kilichochongoka kama mwiba. Taa hawezi kuacha mwiba wake huo kwa kuwa ni sehemu ya maumbile yake Matumizi: methali hii hutumiwa kumnasihi mtu atahadhari na mtu mbaya au anayeweza kumletea madhara
vi) Mtahini aandike kisa kinachodhihirisha mtu anayejihusisha na mtu mbaya kisha aonywe
vii) Mtu mbaya afiche ubaya wake lakini mwishowe audhihirishe huo ubaya wake kwa kumtendea maovu
3) i) Hili ni swali la mjadala
ii) Mtahiniwa aonyeshe hoja za kuunga mkono na zile za kupinga ziweze kutetewa kwa ithibati
iii) Mtahini ahitimishe kwa kuonyesha msimamo wake
iv) Mtahiniwa akishughulikia upande mmoja asipite kiwango cha C+ maki 10
v) Ikiwa hoja za upande mmoja ni nyingi kuliko za upande mwingine atakuwa ameonyesha msimamo wake
vi) Asipoonyesha msimamo wake hilo ni kosa la kimtindo. Hapa ni pale ambapo hoja za kuunga na kupinga ni sawa katika idadi.
Hoja zinazotarajiwa
Hoja za kuunga
i) Vifaa vingi vinavyotumiwa na mwanadamu kuwasiliana husababisha madhara kwa sehemu za mwili wa binadamu k.v rununu huaminika kusababisha saratani, tarakilishi ukiitazama kwa muda mrefu huharibu macho
ii) Watu hutumia muda mwingi kuangalia runinga badala ya kutumia muda huo kujenga taifa
iii) Wezi kutumia teknohama kuwaibia watu
iv) Simu ya rununu imevunja ndoa nyingi kutokana na ujumbe mbalimbali
v) Visa vya uongo / undanganyifu vimeimarika
vi) Vijana hutazama filamo chafu kupitia kwa mtandao
vii) Watoto na vijana kujifunza mambo mabaya kupitia kwa mtandao
viii) Huathiri wanafunzi kwani wengi hupoteza muda mwingi wakiwasiliana kwenye mtandao
ix) Mtandao hutumiwa kueneza fitina, uchochezi na propaganda mbalimbali.
Hoja za kupinga
i) Imerahisisha mawasiliano
ii) Kuimarisha biashara
iii) Imefanya dunia kuwa kama kijiji kimoja
iv) Imerahisisha utendaji kazi kwa kuwepo njia mbalimbali za kuwasiliana
v) Hutoa ujumbe wa moja kwa moja kwa kutumia nukulishi
vi) Burudani kupitia michezo mbalimbali katika ngamizi / utandarithi:
4 Swali la mdokezo
i) Mtahiniwa aandike hadithi juu ya mtu aliyeshtakiwa
ii) Kosa alilolitenda liwahusishe mkewe na wanawe
iii) Apatikane kuwa mkosaji
iv) Hukumu itolewe dhidi ya mshtakiwa na hukumu hiyo iwe kali
v) Mashtaka yalenge ukiukaji wa haki za watoto na wanawake. Kisa kisipozingatia haya mtahiniwa atakuwa amepotoka apate alama ya D maki 03.
vi) Asipokamilisha kwa maneno hayo hajajibu swali Apate D- 02
vii) Akiyaweka mwanzoni au katikati atakuwa amejitungia swali apate D- 02
viii) Akiacha neno au maneno ya kimalizio atakuwa amejitungia swali Apate D- 02
20 marks