Search
Free School Management System
Free School Management System for Kenya

Free School Management System

Learn More

KCSE CLUSTER TESTS 25

Kiswahili Paper 3

1. SEHEMU YA A (Alama 20)

FASIHI SIMULIZI
1.

a. Maana ya miviga Miviga ni sehemu au ibada zinazofuata utaratibu fulani wa kisanaa za maonyesho ya fasihi simulizi. (alama 2)

Inakotumiwa

i. Katika matanga ili kuliwaza wafiwa.

ii. Katika unyago kufunza wari, nasalia na mazingira yao.

iii. Katika mavuno kutoa shukrani

iv. Baada ya vita huwatolea shukrani mashujaa

v. Mtoto anapozaliwa –miviga humkaribisha.

vi. Wakati wa harusi huwapongeza wanacharusi.

vii. Matambiko.

viii. Kutawazwa kwa uongozi. Zozote 8 x 1 = 8

b). Umuhimu wa miviga

i. Hudumisha mila na utamaduni wa jamii.

ii. Huwawezesha vijana kuwa na kumbu kumbu za kila sherehe ilivyofanywa, wakati na maana yake.

iii. Huelimisha vijana.

iv. Hutahadharisha kuhusu maovu.

v. Huwezesha vijana kuelewa au kufahamu desturi zake.

vi. Huleta umoja na ushirikiano katika jamii.

vii. Huburudisha.

viii. Hufundisha unyumba na malezi.

ix. Huhimiza bidii ya kufanya kazi na kujitegemea.

x. Huleta maendeleo. Zozote 5 x 2 =10 Mstahiki

20 marks

SEHEMU YA B (Alama 20)

Tamthilia
2.

Mstahiki Meya

2. Kinyume na matarajio.

i. Anaendesha baraza kwa kutumia uongo – anasema dawa zimeingia.

ii. Analalamikia maswala madogo madogo kama –viyai.

iii. Anapapia chakula hadi ananyongwa na kuchomeka.

iv. Anakataa kuskiza ushauri wa busara wasiku na diwani.

v. Anaifilisi hazina ya Barasa kwa kuidhinisha nyongeza ya mishahara.

vi. Anaiba viwanja vya baraza.

vii. Anaharibu uchumi kuwapeleka wanawe kusomea ng’ambo /mke anazalia ng’ambo.

viii. Badala ya kuboresha elimu anaiona kuwa duni na kuwapeleka wanawe ng’ambo.

ix. Anafuja pesa kwa kujistarehesha katika hoteli za kifahari.

x. Anampokonya mwanakandarasi kandarasi.

xi. Anashawishika kuiba fimbo ya meya.

xii. Anautelekeza mji kwenye uchafu.

xiii. Anatafuta maombi kwa shilingi laki moja.

xiv. Uongozi wake unashindwa kuleta uthabiti wa usalama wa chakula.

xv. Anatumia asasi km polisi kuwatawanya wapigania haki.

xvi. Anamwajiri mzahili ambaye hajahi hitimu zinazofaa.

Mstahiki meya

Muktadha wa dondoo

3a. -Maneno yalisemwa na Beka

-Alikuwa akimwambia Meya.

-Walikuwa afisini mwa Meya

-Meya alikutana na wawakilishi wa wafanyikazi. 4 x 1 = 4

(b). Malalamishi ya mzungumzaji na alioandamana nao.

i. Kutoshughulikiwa kwa maslahi ya wafanyikazi.

ii. Ajira inayojali maslahi yao.

iii. Mshahara wenye kuchelewa.

iv. Vipeni visivyo na manaa kwa mfanyikazi.

v. Ajira wanayoweza kujivunia mbele ya familia.

vi. Hawana hazina – hawaweki chochote.

vii. Mishahara midogo.

viii. Hawapati nyongeza.

ix. Watoto wao wanahitaji kula na kusoma.

x. Wanaambiwa kulipia madawa ilhali madiwani wana bima.

xi. Wanaosha vyoo bila glovu.

xii. Hawana wa kuwatetea katika vikao vya maamuzi

20 marks

SEHEMU YA C. (Alama 20)

RIWAYA : Utengano
3.

4 a. Msemaji ni Biti-kocho

b. Msemewa ni Bi Farashuu.

c. Wako nyumbani kwa Farashuu.

d. Alikuwa akifurahia alivyofaulu kumtalikisha Tamima. na kumtoa Maimuna. Zozote 4 x 1 =

4 (b). Yale msemaji na msemewa waliyofuzu kwayo.

i. Kumtoa Maimuna.

ii. Kumtalikisha Tamima.

iii. Kusambaratisha familia ya Bw. Maksuudi.

iv. Kumchochea Maimuna kuhusu mapenzi.

v. Kusababisha kipigo cha lazima.

vi. Kuvuruga kanuni za nyumba ile kwa kuleta mkunga.

vii. Kumwingiza Maimuma katika ukahaba.

viii. Kulipiza kisasi dhidi ya familia ya Maksuudi.

ix. Maksuudi kuhasimiana na Mussa. zozote 8 x 2 =16.

Utengano

5. matatizo yanayokumba mataifa yanaoendelea ya Afrika.

i. Ufisadi.

ii. Uongozi mbaya.

iii. Tamaa na ubinafsi.

iv. Umasikini.

v. Biashara ya magendo

vi. Ukoloni mamboleo.

vii. Ubaguzi wa kijinsia.

viii. Chuki na uhasama.

ix. Ubabedume

x. Kutowajibika

xi. Tamaduni finyu/hasi

xii. Mizozo ya kifamilia

xiii. Kisasi

xiv. Utabaka

xv. Ulevi
xvi. Ulaghai

20 marks

SEHEMU YA D (Alama 20)

Ushairi
4.

6. Bahari za ushairi

i. Ukaraguni –vina vinabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine.

ii. Kikwamba – Neno chema limerudiwarudiwa katika kuanza kila ubeti.

KUTUZA: Kutaja 2 x 1 = 2

Maelezo 2 x 2 = 4

(b). Umbo la beti mbili za mwisho.

i. Mishororo mine

ii. Vina vinavyobadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine.

iii. Mizani _____6, _____6

iv. Kuna kituo / kimalizio Zozote 2 x 2 = 4

(c). Maudhui

i. Mwandishi analalamika kuwa kitu kizuri hakidumu.

ii. Chema kinamwondoka.

iii. Nyanyake ambaye ni kipenzi chake hatarudi (kaaga).

iv. Mwanawe kafa. Zozote 2 x 2 =4

(d). Matumizi ya tabdila

i. N’ongeza

ii. Kukingojeleza

iii. Kinshaniliza iv. Kinmiondoka.

e. Msamiati

i. Ningetamani – Hata nikimtamani.

ii. Kinakuteleza –kitakuondokea.

iii. Kinshamiliza –kunifanya nilie.

iv. Ela - isipokuwa.

v. Alojipa tabu -aliyejishughulisha.

vi. Hini - hii.

7. ( a). Aina la shairi Tathmina

Lina mshororo mmoja katika kila ubeti

-kutaja alama 1 Maelezo alama 2 Jumla alama 3

b. Umbo la shairi

i. vipande viwili

ii. Mizani ___7__7

iii. Vina vinabadilika

iv. Mshororo mmoja

v. Beti 16 Zozozte 4 x 2 = 8

c. Uhuru wa mshairi

i. Inkisari sie - sisi

lipataje - tulipataje

kutaja alama 1 mifano alama 2 jumla alama 3

ii. Kuboronga sarufi - ni wapi litoka - Ilitoka wapi

Kutaja - alama 1 Mfano - alama 2 Jumla - alama 3

d. Maudhui Mwandishi azungumzia weusi na ubaya wake.

20 marks

SEHEMU YA E (Alama 20)

Hadithi fupi-Damu Nyeusi : Ken Walibora
5.

Muktadha

i. Maneno yalisemwa mwanamke mweusi (Flora).

ii. Alikuwa akimwambia Fikirini.

iii. Walikuwa nyumbani mwa Flora na Bob

iv. Bob alitaka kumpiga bastola huku Flora alitaka kumdunga kisu. Zozote 4 x 1 = 4

b. Dhana waliyokuwa nayo watu wa Marekani kuhusu watu waafrika.

i. Watu hutembea uchi.

ii. Wanaugua ukimwi, malaria, polio, utapia mlo.

iii. Hupigana daima.

iv. Walivaa nguo mara ya kwanza walipokanyaga Marekani.

v. Hawajui mji mkuu wa Afrika.

vi. Weusi unatokana na kuangukiwa na lami au kupigwa na mianzi ya jua.

vii. Wanaishi mitini kama tumbiri.

viii. Waafrika wanaenda kusumbua Marekani.

20 marks

Back Top