Search
Free School Management System
Free School Management System for Kenya

Free School Management System

Learn More

2015 KCSE Murang'a South Mock

Kiswahili Paper 3

1.SEHEMA YA A (Alama 20)

USHAIRI Swali la lazima. Soma shairi kisha ujibu maswali
1.

(a) Bahari - Pindu

(b) (i) Kunyesha usiku na mchana (kutwa kucha)
(ii) Mimea kuharibika.
(iii) Barabara kuharibika.
(iv) Njia hazipitiki.
(v) Watu kutotoka nje. (zozote 4 x 1 = 4)
(c) (i) Mishororo minne katika kila ubeti.
(ii) Mizani 16 katika kila mshororo.
(iii) Kila mshororo umegawika katika vipande viwili.
(iv) Vina vinabadilikabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine. (4 x 1 = 4)
(d) Idhini ya ushairi.
(i) Lahaja m.f sitawata, ndiya
(ii) Inkisari m.f walotenda
(iii) Tabdila m.f mvuwa, iliposiya
(iv) Mazda - kwenenda, maradi (3 x 1 = 3)
(e) Lugha nathari;
Mvua iliyonyesha ya radi na ngurumo kutwa na kucha ilinyesha bila kipimo. Haikuwanufaisha
wakulima kwa kuwa walifikiwa na hasara. (al 4)
(f) Mbinu za lugha.
(i) Taswira - barabara zisizopitika
- barabara zenye matope
(ii) Tashbihi - Mfano wa samaki.
(iii) Takriri - ilitekukatekuka, maneno ya mwisho wa mstari 3, mwanzo wa mstari 4.
(iv) Tashihisi - ikanibwaga telezi
(v) Lahaja - ndiye, sitawata. (zozote 2)
(g) (i) Kutwa na kucha - mchana na usiku.
(ii) Kuicha mvua - kuiogopa.
(al 2)

20 marks

2.SEHEMU B (Alama 20)

RIWAYA. Ken Walibora: Kidagaa Kimwemwozea. Jibu swali la 2 au la 3
2.

Riwaya : Kidagaa Kimemwozea.
(a) (i) Msemaji - Mzee Matuko Weye.
(ii) Msemewa - Imani Mtembezi
(iii) Seli walikofungiwa.
(iv) Amani na Imani wameletwa seli alikofungiwa.
Matuko Weye na anawatetea.
(b) (i) Unyakuzi wa mashamba k.m la akina Amani.
(ii) Watu kusingiziwa makosa kisha kufungwa k.m Yusufu, Amani na Imani.
(iii) Mauaji ya kiholela k.m Chichiri Hamadi.
(iv) Viongizi na washerati k.m Mtemi Nasaba Bora.
(v) Ubadhirifu wa pesa za umma k.m Fao alipelekwa ng’ambo kwa pesa zilionuiwa kulipia watoto wa
maskini.
(vi) Kodi za lazima k.m Mtemi Nasaba Bora aliwatoza pesa kwa lazima ampeleke mwanawe Urusi
kusoma.
(vii) Mapendeleo k.m Nasaba Bora alihonga wakuu wa jeshi mwanawe apate cheo jeshini.
(viii) Ufisadi k.m Mtemi Nasaba Bora alibadilisha hatimiliki za mashamba ajilimbikizie.
(ix) Mahakama kutoa uamuzi usio wa haki k.m Yusufu anafungwa kwa visingizio.
(x) Dhuluma kwa waandishi k.m mswada wa Amani kuchapishwa kwa jina la Majisifu.
(zozote 6 x 2 = 12)
(c) Sifa za mnenaji.
(i) Mwanamapinduzi.
(ii) Mpenda haki.
(iii) Jasiri / mkakamavu
(iv) Mwenye urazini / amezinduka.

(v) Mtetezi wa haki.

20 marks

3.

(i) Sadfa - Mambo kutokea kwa pamoja bila kupangwa. k.m
- Kukutana kwa Amani na Imani kando ya ziwa Mawewa.
- Kukutana kwa Amani, Imani na D.J kando ya Mto Kiberenge.
- Amani anapotafuta kazi kwa Mtemi mchungaji wa awali ni mgonjwa na hawezi kuendelea na kazi n.k.
- Kifo cha Uhuru kinasadifiana na Majisifu kuja kumtafuta Imani arejee kazini kwake.
- Bi zuhura anapamwita Amani chumbani, mumewe anaingia.
(ii) Barua.
- Ni mbinu ya mawasilianao kwa njia ya maandishi.
- Barua ya Madhubuti kwa babake.
- Barua ya Lowela kwa Mtemi Nasaba Bora.
- Barua ya Ben Bella kwa Mashaka.
- Barua ya Majisifu ya ualishi chuo cha wangwani..
- Barua ya Amani kwa Imani.
(iii) Jazanda.
- Ni ujumbe uliofumbwa.
- Fahali kula kaptula ya DJ na kumwacha bila chochote -Mtemi Nasaba Bora kunyakua mashamba ya maskini na kuwaacha bila.
- Kutokufa kwa wakereketwa / wanamapinduzi k.m Amani, DJ na Imani ni kutofifisha mapambano ya
ukombozi.
- Ndoa ya Amani na Imani ni mwanzo wa ujenzi wa jamii mpya.
- Kifo cha kitoto Uhuru ni uhuru wa nchi ya mkoloni kuondoka. Tomoko haukupewa nafasi ushamiri.
- Kifo cha Mtemi Nasaba Bora ni mwisho wa uongozi mbaya.
- Jibwa Jimmy ni mkoloni mkongwe ambaye athari yake inahisika.
- Safari ya Amani kwenda Sokomoko ni safari ya kusaka haki na ukweli. (zozote 4 x 1)
(iv) Mbinu rejeshi/kisengere nyuma /Matukio ya awali kuletwa mbele.
- Amani na Imani walivyokutana.
- Amani alivyosingiziwa akiwa chuoni kishakufungwa.
- Imani akielezea walivyonyang’anywa shambalao.
- Mtemi akieleza alivyopanga mauaji ya Chichiri Hamadi.
- Imani anakumbuka kisa cha Majununi.
- Jinsi Nasaba Bora alivyonunua mkweche wake na mauaji ya paka.
- Sababu za marukufu ya kunywa maji ya mto
Kiberenge. - Maelezo ya mbinu alama 1
- Mifano ya mbinu alama 4
(4 x 5 = 20)

20 marks

3.SEHEMU C (Alama 20)

TAMTHILIA Timothy Arege: Mstahiki Meya Jibu swali la 4 au la 5
4.

(i) Sheria kandamizi k.m Mayor’s Act na Riots Act.

(ii) Propaganda za viongozi - mf: Waandamanaji hawakuukawa.
(iii)Ushauri wa kupotosha.
(iv) Ubinafsi wa viongozi.
(v) Matumizi ya vyombo vya dola k.v askari kutibua maandamano.
(vi) Ujinga wa wananchi kuchagua viongozi wabaya.
(vii)Wananchi waadilifu kukataa kuwania uongozi.
(viii)Mapendeleo k.m madiwani na askari kuongezewa mishahara wamuunga mkono Meya.
(ix)Unafiki wa kidini k.m Meya kuita mhubiri kuombea baraza lililojaa uovu aonekane ni mcha Mungu.
(x) Uzalendo bandia k.m nyimbo za kizalendo baada ya vipindi maarufu.
(xi) Kutengwa kwa viongozi waadilifu k.m Diwani wa III
(xii)Ahadi za uongo kuwapa watu moyo wa matumaini au subira.
(xiii)Upurukushani k.m Dida kutojali. (zozote 10 x 2 = 20)

20 marks

5.

Daktari Siki.
- Anapeleka malalamiko ya kucheleweshwa kwa dawa kwa Meya.
- Anawapa wagonjwa matumaini.
- Anatahadharisha wawakilishi wa wafanyikazi dhidi ya hatari za migomo.
- Anaendelea na kazi licha ya hali gumu za kikazi k.v mshahara mdogo, tishio la maambukizi mahali pa kazi
n.k.
- Anashirikiana na Diwani wa III kutafuta suluhisho la matatizo ya wanacheneo.
- Anahimiza wafanyikazi waendelee kutetea haki zao.

Anawahamasisha wanacheneo watetee haki zao k.m Meya anamuuliza kama alichochea mgomo mwingine.
- Anamueleza Meya ukweli wa mambo kuhusu hali ilivyo Cheneo (zozote 5 x 2 = 10)
Diwani wa III.
- Anatetea haki za wafanyikazi waongezewe mishahara pamoja na viongozi.
- Anapendekeza kodi itozwe hata viongozi ili kuimarisha uchumi wa baraza.
- Analalamikia kutengwa katika maamuzi muhimu ya baraza k.v kuidhinisha nyongeza ya mishahara.
- Anaonyesha heshima kwa Meya kwa kuzingatia dhana ya Collective responsibility.
- Anashirikiana na daktari Siki kutafuta suluhu ya matatizo ya wanacheneo.
- Anamzindua Siki kuwania uongozi kuleta mabadiliko.
- Hakubaliani na maoni ya madiwani wenzake.
- Anampinga Meya katika mapendekezo anayoona hayafai. (zozote 5 x 2 = 10)

20 marks

4.SEHEMU D (Alama 20)

HADITHI FUPI Ken Walibora: Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine.
6.

Hadithi Fupi: Damu Nyeusi na Hadithi Nyingine
i) Hali ngumu ya maisha / umaskini – inamfanya Kananda kutafuta kazi kwa Bw. Mwatela ambako
anapachikwa mimba (mwana wa Darubini)
ii) Abu anakosa msichana wa kuoa kila anapopeleka posa (Ndoa ya Samani)
iii) Ulimbukeni wa mapenzi unawafanya wasichana kupata mimba wakiwa shuleni k.m Sela na wasichana
wenzake watatu (kanda la usafi)
iv) Christine anapata mimba akiwa chuoni. (Samaki wa Nchi za Joto)
v) Shinikizo la marafiki linafanya kina Semkwa wavamiwe. k.m Semkwa (Glasi ya mwisho)
vi) Kupuuza ushauri k.m Christine (Samaki wa Nchi za Joto)
vii) Tamaa ya maisha ya hadhi k.m Chritine (Samakiwa Nchi za Joto),Lucy katika Tazamana na
Mauti.
xiii)Ubaguzi wa rangi k.m Fikirini (Damu Nyeusi)
ix) Kutegemea wazazi k.m Amali kukosa mume. (Ndoa ya Samani)
x) Woga k.m Kananda kutishiwa na Mwatela kisha k unyang’anywa mtoto (Mwana wa Darubini)
xi) Ukatili wa wazazi k.m Sudi kutupwa na mamake
(Mizizi na Matawi)
xii) Tabia ya kidomo na kimbelembele k.m Seruwa alikosa kuolewa na msimulizi (Mke Wangu).
xiii)Ufuska na anasa k.mChristine (Samaki wa Nchi za Joto) (zozote 1- x 2 = 20)

20 marks

5.SEHEMU E (Alama 20)

FASIHI SIMULIZI.
7.

(i) Ngomezi - maana.
(i)- Ni fasihi ya ngoma. Huhusisha ala za muziki kupasha ujumbe.
(ii) - Fasihi ya ngoma na ala zingine za sauti. yoyote 1 x 2 = 2
(ii) Sifa za ngomezi.
- Mdundo wa ala hueleweka na wenyeji / jamii husika.
- Huwa na ala.
- Midundo ya ala ina maana maalum.
- Huongozwa na watu maalum (masogora)
- Hutenga hadhira teule.
- Ni ya wakati maalum zozote 6 x 1 = 6
(iii) Dhinia / majukumu ya ngomezi.
- Kuburidisha wakati hakuna tukio zito.
- Kukuza ustadi k.m Masogora huonyesha ubingwa katika kutumia ngoma kuwasilisha ujumbe.
- Kuficha ujumbe usifahamike na wasiohusika.
- Kuharakisha mawasiliano.
- Hutahadharisha.
- Hudumisha utamaduni.
- Hudhihirisha ufundi wa kisanaa.
- Kuipa jamii utambulisho.
- Kukuza mila na desturi.
- Husaidia kwenye sehemu zenye mawasiliano magumu.
- Hutoa matangazo rasmi kuhusu jambo.
- Kufahamisha kunapotokea jambo lenye uzito. (zozote 6 x 2 = 12)

20 marks

Back Top